Saturday 18 June 2016

MWIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI TANZANIA ANDREW KIWHELO ALIVYOWEZA KUSEMA YALIYOMOYONI MWAKE KUHUSIANA NA KITUO CHA RADIO PRAISE POWER RADIO

Mwimbaji wa nyimbo za Injili Andrew Kiwhelo aliweza kufika katika studio ya Rumafrica na kuweza kusema machache kuhusiana na Redio Praise Power 99.3FM alikuwa na haya ya kusema,
Bwana Yesu apewe sifa watu wa Mungu. Kwa jina naitwa Andrew Kiwhelo mwimbaji wa nyimbo za Injili Tanzania na mzaliwa wa Iringa ila naishi jijini dar es Salaam, nimeoa mke mzuri na mpenda kutoka nchini Kenya. Leo hii nipo mahali hapa kuelezea jinsi navyoifahamu redio ya Praise Power 99.3FM ambayo iko chini ya Bishop Dr. Gertrude Rwakatare wa kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni “B” jijini Dar esa salaam Tanzania.
Mwimbaji wa nyimbo za Injili Tanzania, Andrew Kiwhelo (kushoto) na mtangazaji wa Praise Power Radio 99.3FM Ben Bonge na Rumafrica Lets Talk katika studio ya Rumafrica

Binafsi nimeifahamu Praise Power Radio kipindi nipo kwenye bendi moja ya muziki ambayo siwezi kutaja jina kwa sasa. Nakumbuka siku moja katika harakati zetu za kutaka kuzitangaza nyimbo zetu redio, tuliamua kukaa chini na waimbaji wenzangu na kuamua kupeleka nyimbo zetu Praise Power Radio ili zipigwe na kusikika na watu wengina nah ii  ilikuwa ni mwaka 2004 au 2005

Praise Power Radio imefanyika faraja kubwa sana katika maisha yangu na pia kwa Watanzania walio wengi. Mimi kipindi hicho cha nyuma nilikuwa mshiriki wa kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni “B” na nimeona uzuri wa hii redio.

Nimebahatika kusikiliza redio nyingi sana hapa Tanzania lakini Praise Power Radio imekuwa faraja sana kwangu ukifananisha na redio zingine. Redio hii imekuwa haibagui aina ya watumishi wa Mungu. Kwetu sisi waimbaji tumekuwa tukipata ushauri kutoka kwa watangazaji tunapopeleka nyimbo zetu redio, na pale ambapo kuna upungufu wamekuwa wakitushauri cha kufanya ili kuboresha huduma yetu ya uimbaji.

Tunamuomba sana Mungu azidi kumbariki sana Bishop Dr. Gertrude Rwakatare kwa maono ya kuanzisha kituo hiki cha redio. Kupitia redio hii mimi nimeweza kufahamika na watu wengi sana kuanzia ile albamu yangu ya kwanza na ile ya pili, hakika wameweza kusimama na mimi tangia kipindi hicho cha nyuma mpaka leo hii. Praise Power redio imenisaidia sana kwa mambo mengi mno ambayo mengine siwezi hata kuyataja.

Ningependa kushauri kwa yeyote ambaye amewahi kusikiliza Praise Power Radio 99.3FM na Yule ambayo nib ado wajitahidi sana kuendelea kusikiliza redio hii kwa kuna vipindi vya kukuelimisha kutoka kwa watangazaji ambayo wamejitoa kufanya kazi ya BWANA na wamejipanga vizuri pia wanajituma kumtumikia Mungu kwa unyeyekevu sana.

Mimi binafsi ninapenda sana vipindi vya Praise Power Radio 99.3FM hasa kipindi cha Rise and Shine chini ya Veronica Frank, Kesha na Praise Power chini ya Erick Brighton na John Kissaka, Sifa Moto chini ya Bony Magupa, Jamvi Chini ya Ben Bonge, Joyce na Frida, pia kipindi cha Power Drive ambacho huzungumzia nchi yetu ya Tanzania kwa undani zaidi, Faraja Time chini ya Victor Aron

Kuna watu wengi sana wanabarikiwa sana na vipindi vya Praise Power Radio, watu wanapokea miujiza yao na uponyaji wanaposikiliza watangazaji na watumishi wa Mungu wanahubiri kupitia redio hii

Watangazaji wamejipanga vizuri na katika mazungumzo yao wanatoa maneno ya faraja kutoka kwenye Biblia. Radio ya Praise Power haichagui rangi, kabila, taifa wala jinsia, ni radio ya watu wote.

Mwisho nataka kuwajulisha kuwa nyimbo zangu unaweza kusikia katika redio hii ya Praise Power Radio 99.3FM na albam yangu mpya ya BUSH TO TOWN inapatikana sokoni kwa sasa. Kwahiyo ukitaka kusikiliza nyimbo zangu kama vile ONEKANA LEO na nyingine nyingi usikose kusikiliza hii redio ambayo ni mkombozi wetu katika kutangaza kazi na huduma zetu.


Ukitaka kunipata mimi na ukatamani kunialika kwenye mkutano, semina, kongamano au tukio lolote la kumtukuza Mungu basi wasiliana name kwa simu hizi, o716 470 104 au 0763 416 382, Mungu akubariki sana na endele kusoma Gazeti Rumafrica Online Magazine, Kusilikiza Praise Power Radio na kuangalia Rumafrica Online TV pamoja na Mlima wa Moto TV. Nakupenda

Wednesday 25 May 2016

UPDATES KUTOKA PRAISE POWER Online MAGAZINE














ALIYEKUWA MCHAWI MWENYE MAJINI 25 SAFI NYEULA (MWAROBAINI) MKAZI WA GEZAULOLE NURUNI KIGAMBONI AACHANA NA UCHAWI NA KUOKOKA


Bwana apewe sifa. Habari njema kutoka kanisa jipya la Mlima wa Moto Gezaulole Nuruni Kigamboni. Kama kanisa mmekuwa mkijitoa sana katika upanuzi wa kanisa letu la Gezaulole Kigamboni, nami napenda kuwashukuru sana na najitahidi kuleta matunda yanayotokea katika kanisa letu jipya kwa msaada wa Mungu. Watu wanazidi kuokoka na kuacha uchawi na uganga. Mpaka sasa kanisa limeshasimama na sasa wanahangaikia nzege.
 
Kutoka kushoto ni Bishop Dr. Gertrude Rwakatare, Safi Nyeula na mhudumu wa kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni "B"

Na leo tumemuleta Safi Nyeula ambaye alikuwa mchawi wa kutisha Kigamboni. Ngoja usome ushuhuda wake:-

Baada ya hapo mama Safi alikuwa na haya ya kusema, “Bwana Yesu asifiwe, kwa jina ninaitwa Safi Nyeula, kwetu ni Musoma lakini mimi ni mtu wa bara. Kwa jina lingine ninaitwa Mwarobaini, hili ni jina gumu sana. Mimi ni mtoto mdogo sana lakini matendo yangu yalikuwa ni makubwa. Nilikuwa na majini 25, nilikuwa na makuu upande wa baba yangu na upande wa mama yangu na mengine, nilikuwa na vitambaa vyote (chekundu, cheupe na cheusi). 
Kitambaa cheusi nilikuwa navaa upande wa mamimi (yakipanda mashetani naongea cha kwetu, akipanda kisimba navaa kitambaa chekundu, akipanda Shariff navaa kitambaa cheupe na akipanda maimuna navaa cheusi ), Nikitaka chochote nilikuwa navaa vitambaa hivyo na ninapandisha mashetani na ninaongea. Kama unashida yoyote ninakuambia na ninakutibu, kama akina mama wanahitaji wapenzi, wanaohitaji biashara, mume asimnyayase mimi nilikuwa natibu. Nilikuwa na uwezo wa kujaza samaki kwenye mitubwi ya wavuvi hasa waziwa. 
Mwaka 2002 nilianza kuugua, na nikaenda makanisa mengi bia kupata uponyaji. Walikuja wachungaji kutoka Arusha wakitaka niokoke lakini nilikataa nikawaambia ukifika wakati nitaokoka. Nilikuwa naumwa majini, na nikianza kuugua, miguu (magotini), tumbo, kifua, kichwa vinauma sana mpaka inafika point nasema, ni heri nife. 
Nilikuwa natumia pesa nyingi kwa madaktari lakini sipati uponyaji (kweli daktari hajigangi). Mimi nilikuwa ni mlevi sana, nakunywa pombe kuanzia asubuhi hadi jioni na silewi kamwe, ninaweza nikafululiza siku tatu ninakunywa pombe. 
Nikinywa hiyo pombe nilikuwa simuogopi mtu yeyote yule. Nilikuwa napiga watu na nikikupiga lazima utoke damu na ilikuwa haiwezekani nikakupiga usitokwe na damu. Na nimebahatika kuwa na mume wangu na watoto watatu. 
Lakini sasa ninamshukuru Mungu kwa kutuletea Bishop Dr. Gertrude Rwakatare Gezaulole Kigamboni ambaye amekuja kutuokoa na mkuu wetu wa majini alikuwa Kasimu Suleiman. Ndugu zangu walikuwa wanasema hawadhani kama ninaweza kusimama kwenye wokovu, lakini sasa kwa nguvu aliyonayo mama Gertrude Rwakatare nimesimama. 
Siku ya tatu ya  semina ya ufunguzi wa kanisa jipya la Gezaulole nilimuomba kaka yangu twende naye na vitu vyangu vya uchawi nikavisalimishe kwa Yesu. Nilipofika pale nikachoma vitambaa vyote na maajini yote kama jini sharifu, jini makata, jini maimuna, jini masai, jini bubu. Jini Masai likija lazima uvae kimasai. 
Nichotaka kuwambia ndugu zangu kuwa mmkiri huyu Yesu Kristo, na inabidi msikae nayo mizigo ndani na mkikaa nayo mnazidi kudidimia, mtatoka kanisa lakini bado nyumbani mna msalaba ule ule. Mungu awabariki sana

Facebook: Mountainoffire Tanzania